Posts

HABARI YA KIUCHUMI

Image
 Wafugaji wa Ng'ombe wa maziwa wametakiwa kutumia njia bora za kufanya uwekezaji huo ili uwe unatija kwao kwa kuzingatia maelekezo ya wataalamu wa mifugo waliopo hapa nchini.   Ameyasema hayo wa Mwanafunzi wa skuli ya kilimo na ufugaji kizimbani wilaya ya magharib A Unguja Neema Omar Mwalim,Alieleza ili ufugaji wa Ng'ombe wa maziwa uwebora ni vyema jamii ikajenga tabia ya kufuata ushauri wa wataalamu wa mifugo .  Alisema wafugaji wa hapa nchini wanatakiwa kuzijua njia za kuwatunza Ng'ombe wa maziwa kwa vile wanahitaji matunzo mazuri katika ukuaji wake .    Alifafanua kwa kina njia tatu zaufugaji wa Ng'ombe na zikiwemi mbili zinazotaka kuwapa matunzo wanyama hao ili waweze kukuwa vizuri.  Alisema ufugaji wa Ng'ombe unahitaji kuwekwa katika kizuizi ambacho kitawapa hewa katika eneo kubwa ili waweze kujitaftia chakula wenyewe

HABARI ZA KIJAMII

Image
  MASHEHA WAJENGEWA AFISI  Masheha katika shehiya mbalimbali wametakiwa  kuzitumia ofisi zao walizojengewa kwa lengo kutatua kero za wananchi katika shehiya zao   Tamko hilo limetolewa na waziri wa nchi ofisi ya raisi tawala za mikoa serekali za mitaa na idara maalumu za smz mheshimiwa Masoud Ali Mohammed wakati akizindua ofisi  64  za masheha zilizojengwa unguja na pemba huko katika shehia ya matetema wilaya kazkazin B, amesema serikali itaendelea kujenga miundombinu rafiki kwa watendaji wake kwa lengo la kuomarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi    Aidha amewataka masheha hao kuzitumia ofisi hizo kwa ajili ya wananchi  ili kutatuwa changamoto zinazowakabili katika maeneo yao  Katibu mkuu  ofisi ya raisi tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz  issa  mahfudhi haji akitoa   taarifa ya kitaalamu amesema serekali inatarajia     kujenga ten  kwa awamu nyengine ...

HABARI ZA KITAIFA

Image
  waziri wa nchi afisi ya raisi kazi uchumi na uwekezaji zanzibr mheshimiwa shariff ali shariff amezitaka taasisi za umma na za serekali kujiepusha na rushwa na kufuata misingi ya utawala bora ili kuhakikisha kila mwananchi kupata huduma bora . Tamko hilo amelitoa wakati akifungua jukwaa la watendaji wakuu wataasi za umma zanzibr golden tulip uwanja wa ndege ambapo watajadili mada mbali mbali zitakuza taasisi hizo , Amesema endapo taasis za umma watashiriki ipasavyo katika jukwaa hilo itasaidia kutoa huduma bora kwa jamii na kuendana na techonologia ya kisasa ambayo itasaidia kuleta mabadiliko ya maendeleo. Kurugenzi mtendaji zeea juma burhan muhhamed amesema mkutano huo utasaidia kubadilishana mawazo katika taasisi za umma na kutengeneza fursa za kibiashara zitakazo leta maendeleo makubwa katika nchinch Hata hivyo amesema jukwaa hilo litajadili majawabu ya changamoto ya taasisi hizo na kuweka mtandao madhubuti wa wakuu wa taasisi kwa kubadilishana uzoefu maarifa na mbinu bora z...

HABARI ZA KISIASA

Image
 Chama cha Act wazalendo Zanzibar kimelaani vikali kauli ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Idris Kitwana Mustafa kuhusu agizo lake la hivi karibuni la kuwataka watumishi wa ofisi yake na watumishi wa umma katika mkoa huo  kumuwasilishia vitambulisho vya kupigia kura . Akizungumza na Waandishi wa habari huko katika ofisi za makao makuu ya chama hicho Vuga Mjini Zanzibar mwanasheria mkuu wa chama hicho ndugu Omari Saidi Shaabani. Alisema Kitendo hicho ni kinyume na katiba na sheria za nchini  huku  akikiita  Kitendo hicho kua ni kosa la jinai. Alisema RC Kitwana amejivika mamlaka yasiyokua ya kwake kisheria kutokana na mihemko ya kisiasa ambayo yanampelekea kuvunja Sheria katika nchi.  Alisema kauli hizo za Kitwana zinakiuka Sheria tano mbali mbali katika nchi jambo ambalo linashajihisha uhalifu, jinai na kutia hofu wananchi. Akizitaja Sheria hizo ni pamoja na sheria ya uchaguzi ya Zanzibar na Tanzania, Sheria ya ulinzi wa taarifa binafsi, sheria ya maa...

HABARI YA NJE

Image
 BALOZI MBUNDI AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KATIKA MKUTANO WA MAKATIBU WAKUU WA EAC Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen P. Mbundi leo tarehe 8 Mei, 2025 ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kikao cha Makatibu Wakuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kinachofanyika jijini Arusha. Kikao hicho na kikao cha maafisa waandamizi wa EAC kilichofanyika kuanzia tarehe 5 hadi 7 Mei, 2025 sehemu ya maandalizi ya Mkutano wa 25 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya hiyo utakaofanyika tarehe 9 Mei, 2025. Kikao hicho cha Makatibu Wakuu kinaangazia vipaumbele vya sekta ya afya katika Jumuiya ikiwemo: Maboresho ya mifumo ya afya inayosomana, ushirikiano katika uchunguzi wa magonjwa ya milipuko na ya kuambukiza, upatikanaji wa teknolojia ya kisasa na bora katika huduma za afya na uimarishaji wa mfumo wa usimamizi wa sekta ya afya. Akitoa salamu za Serikali katika ufunguzi...