HABARI ZA KIJAMII

 MASHEHA WAJENGEWA AFISI 



Masheha katika shehiya mbalimbali wametakiwa  kuzitumia ofisi zao walizojengewa kwa lengo kutatua kero za wananchi katika shehiya zao  

Tamko hilo limetolewa na waziri wa nchi ofisi ya raisi tawala za mikoa serekali za mitaa na idara maalumu za smz mheshimiwa Masoud Ali Mohammed wakati akizindua ofisi  64  za masheha zilizojengwa unguja na pemba huko katika shehia ya matetema wilaya kazkazin B, amesema serikali itaendelea kujenga miundombinu rafiki kwa watendaji wake kwa lengo la kuomarisha utoaji wa huduma bora kwa wananchi  

 Aidha amewataka masheha hao kuzitumia ofisi hizo kwa ajili ya wananchi  ili kutatuwa changamoto zinazowakabili katika maeneo yao 

Katibu mkuu  ofisi ya raisi tawala za mikoa serikali za mitaa na idara maalum za smz  issa  mahfudhi haji akitoa   taarifa ya kitaalamu amesema serekali inatarajia     kujenga ten  kwa awamu nyengine  ofisi  48 katika shehia zote 388 zikiwa na vifaa vya kisasa.

Mkuu wa mkoa wa kazkazin unguja mheshimiwa  Matar zahaour masuod amesema.katika mkoa huo kuna ofisi kumi na mbili ambzo zitasaidia kuweka mazingira mazuri baina ya wananchi na masheha .

Nao masheha wa shehia mbali mbali wamesema ofisi hiz zitasadia kuondoa changamoto ambazo zilikua zinawakabili katika kazi zao .

Comments

Popular posts from this blog

HABARI YA KIUCHUMI

HABARI ZA KISIASA

HABARI YA NJE